Author Name: GlobalVoices.
(C) GlobalVoices.org
This unaltered story was originally published on GlobalVoices.org.[1]
Republishing Guidelines:
url:
https://globalvoices.org/about/global-voices-attribution-policy/
--------------------
Serikali ya Angola Yafungia Kituo cha Runinga cha Kibrazili kwa Madai ya ‘Kukiuka Taratibu’ [1]
['Global Voices Lusofonia']
Date: 2021-06-13 14:54:09+00:00
Mapema tarehe 19 Aprili, serikali ya Angola ilisimamisha matangazo ya Record TV África, kituo cha kibrazili cha Runinga kinachomilikiwa na kampuni ya Grupo Record, kwa kile kinachoaminika kuwa ni ukiukwaji wa taratibu.
Taarifa rasmi iliyotolewa na Wizara ya Mawasilino, Teknolojia ya Habari na Media ya Angola (MINTTICS)ilieleza kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Record TV África hakuwa mzawa wa Angola. Wizara iliongeza kuwa, wanahabari wa kigeni katika kituo hicho cha runinga hawakuwa na vibali rasmi vya kufanya kazi nchini Angola.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara, shughuli za kituo hiki zilisitishwa rasmi tarehe 21 Aprili, hadi hapo taarifa nyingine itakapotolewa.
Tarehe 30 Aprili, Record TV África ilieleza kuwa ingemadilisha Mkurugenzi Mtendaji, ndugu Fernando Teixeira, ambaye ni raia wa Brazili na kumuweka ndugu Simeão Mundula, ambaye ni raia wa Angola. Kituo hiki cha Runinga kiliweka bayana pia kuwa, hakikuwa kimewaajiri waandishi wa habari ambao hawakuwa raia wa Angola.
Wakati kituo kiki kinasimamishwa, Record ilikiambia kituo kimoja cha utangazaji cha kibrazili kuwa kilishangazwa na maamuzi haya. Kilisema:
Em 19/04/2021, a Record TV Africa foi surpreendida com um comunicado da Direção Nacional de Informação e Comunicação do Ministério das Telecomunicações, Tecnologias de Informação e Comunicação Social (“MINTTICS”).
A Record TV Africa exerce a sua atividade em Angola desde 2005 e conta com atualmente 73 colaboradores diretos e indiretos.
A Record TV Africa, no estrito respeito da Constituição e da lei Angolana, informa o público, parceiros comerciais e, em particular, as suas centenas de milhares de telespectadores diários.
A Record TV Africa, pauta e sempre pautou pela legalidade nos mais de 15 anos presentes em Angola e em todo continente Africano, e irá juntos aos órgãos de tutela buscar o esclarecimentos referente as supostas irregularidades alegadas.
[END]
(C) GlobalVoices
Licensed under Creative Commons Attribution 3.0 Unported (CC BY 3.0)
[1] Url:
https://sw.globalvoices.org/2021/06/serikali-ya-angola-yafungia-kituo-cha-runinga-cha-kibrazili-kwa-madai-ya-kukiuka-taratibu/
via Magical.Fish Gopher News Feeds:
gopher://magical.fish/1/feeds/news/globalvoices/